Saturday, 28 June 2014

 MAKAMU WA RAISI ALGENTINA ASHITAKIWA


 


Makamu wa raisi nchini Argentina Amado Boudou ameshitakiwa na shitaka la ufisadi.

Bwana Badou anashutumiwa kwa kutumia vibaya mamlaka wakati alipokuwa waziri wa uchumi alipochukua umiliki wa kampuni inayochapisha fedha za Argentina.

Washitakiwa wengine watano pia wameshitakiwa kwa kosa hilo .
Bwana boudou kwa mara kadhaa amepinga mshtaka dhidi yake huku akifutilia mbali wito wa kujiuzulu.Kwa sasa yuko katika ziara ya kibiashara nchini Cuba.

Monday, 23 June 2014

WAANDISHI AL JAZEERA WAHUKUMIWA MIAKA 7 JELA



Mahakama nchini Misri imewahukumu jela miaka saba wandishi watatu wa habari wa shirika la habari la Al Jazeera waliokuwa wamezuiliwa kwa miezi sita nchini humo.
Walipatikana na hatia ya kueneza habari za kupotosha na kushirikiana na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Muslim Brotherhood.
Mmoja wa wandishi hao ni Peter Greste, raia wa Australia na ambaye pia alikuwa mwandihi wa habari wa BBC wakati moja.
Hukumu ilipotolewa, Greste kwa hasira aligonga mkono wake katika eneo ambako walikuwa wamezuiliwa huku mwenzake akibururwa kutoka mahakamani na walinzi wa gerezani.

Familia za watuhumiwa nao wakaangua kilio. Kesi hii imelaaniwa sana kote duniani hasa na mashirika ya kutetea haki za binadamu pamoja na mashirika ya habari ya kimataifa.
Lakini nchini Misri, vyombo vya habari vilipeperusha habari hiyo kwa utofauti mkubwa.

Al Jazeera - ni shirika linaloonekana kuunga mkono vuguvugu haramu la Muslim Brotherhood na kwa mtanzamo huo , ni adui wa serikali.
Peter Greste ,ndiye alikuwa anaripoti matukio nchini Misri Disemba mwaka jana wakati wa harakati za mapinduzi.

Kisha yeye na wenzake wawili wakatuhumiwa kwa kusaidia vuguvugu la kigaidi na kutangaza taarifa za kupotosha dhidi ya serikali na maslahi ya taifa hilo.
Madai ambayo serikali ya Australia imekuwa ikikanusha vikali.

Serikali ya Australia ilitoa taarifa yake ikisema kuwa imeshtushwa sana na uamuzi wa mahakama katika kesi ya Peter Greste. Imeelezea kushangazwa sana na hukumu iliyotolewa. Serikali imesema haielewi kabisa matukio haya.

Shirika la Al Jazeera lenyewe limepinga hukumu iliyotolewa dhidi ya wandishi hao, Peter Greste, Mohamed Fahmy na Baher Mohamed likisema kuwa inakiuka sheria.

TAASISI YA AFYA YASHAMBULIWA NIGERIA


Mlipuko umeripotiwa kutokea katika taasisi moja ya umma ya mafunzo ya afya katika mji wa Kano ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini Nigeria.

Duru zinasema kuwa idadi ya watu waliojeruhiwa katika shambulizi hilo dhidi ya kituo cha mafunzo ya afya , bado haijulikani.
Mji huo umewahi kulengwa na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram, ambao wanataka kubuniwe taifa la kiisilamu Kaskazini mwa Nigeria.

Majimbo matatu Kaskazini mwa Nigeria bado yapo chini ya sheria ya hali ya hatari kufuatia miaka mingi ya harakati za wapiganaji hao wa kiisilamu.


Friday, 23 May 2014


 

 WANANCHI WAMLIPUA LISSU KWA KINANA


Wananchi wa Jimbo la Singida Mashariki, wamemuomba Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, awasaidie kutatua kero zinazowakabili za barabara, elimu na afya.

Wananchi hao wamedai hatua ya kumuomba Kinana awasaidie inatokana na Mbunge wao, Tundu Lissu (Chadema), kuwakataza kuchangia miradi ya maendeleo hali iliyosababisha miradi ya ujenzi wa shule na zahanati kusimama kwa kipindi cha miaka minne.

Wakizungumza jana wilayani Ikungi mkoani Singida, mbele ya Kinana, wananchi hao walisema Mbunge huyo amekuwa akiwakataza kuchanga fedha kwa ajili ya kujenga madarasa na majengo ya zahanati kwa madai kuwa serikali ina fedha za kutosha za kufanya kazi hizo.

“Ndugu Kinana tunaomba utusaidie kwani tangu tulipomchagua Mbunge wetu, Tundu Lissu, hajaendeleza miradi ambayo ilianza kufanywa na Mbunge wa CCM aliyepita, baada ya yeye kutukataza kuchanga aina yeyote ya michango itakayotakiwa na halmashauri kwa ajili ya maendeleo, tumeendelea kuwa katika hali ya ufukara” alisema Omary Lissu mkazi wa kijiji cha Unyanghumpi.

Alisema tangu wamekatazwa kutoa fedha za miradi hakuna kazi ambayo imeendelea hasa katika zahanati Kimbwi ambayo walitarajia iwe imeanza kutumika tangu mwaka 2011 lakini hadi sasa bado haijakamilika na kwamba diwani wao amekuwa akiwashinikiza kutoshiriki shughuli hizo.

Naye Mwalimu wa Shule ya Msingi Unyanghumpi, Juliana Joseph, ambaye anafundisha darasa la awali, alisema tangu madarasa hayo yajengwe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, mpaka sasa hakuna majengo mengine mapya wala ya zamani kumaliziwa hali inayowafanya baadhi ya wanafunzi kusoma katika darasa ambalo halijaezekwa.

“Ni mwaka wa nne nafundisha katika darasa hili ambalo halina paa,  na mvua inaponyesha inatubidi tusiudhurie vipindi. Mbunge wetu na diwani walitoa tamko la kuwataka wananchi wasichangie umaliziaji wa jengo ndiyo maana hadi sasa tuko hapa, wala hajawahi kufika kutoa msaada wowote,” alisema Joseph.

Alisema darasa la awali lina jumla ya wanafunzi 135 ambao wote wanakaa kwenye vumbi kwani hakuna madawati na vifaa vingine kama dhana za kufundishia. Mkazi mwingine alisema wamekuwa wakipata tabu ya kufuata huduma ya afya katika kijiji kingine wakati kijijini hapo kuna zahanati ambayo imejengwa inasubiri kukamilika.

Akizungumza na wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Makyungi, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kiongozi bora ni yule anayechangia maendeleo ya wananchi na siyo kuwakataza wananchi kufanya maendeleo.

Alisema Tundu lissu anafanya mambo ambayo hayaendani na matarajio ya wananchi kwani walimchagua wakiamini ataleta maendeleo badala yake anazuia maendeleo. Kwa upande wake, Kinana, alimtaka Lissu kuacha porojo za majukwaani na arudi kwa wananchi kuwatimizia ahadi alizotoa kwani anafedha nyingi anazopatiwa bungeni.

Alisema wilaya ya Ikungi iko nyuma kimaendeleo ikilinganishwa na wilaya nyingine nchini sababu kubwa ikiwa ni mbunge mwenyewe ambaye ameshindwa kupigania maendeleo ya jimbo lake na badala yake amekuwa akigombana na kila mtu serika
lini.

  UN YASEMA VATCAN INAPUUZA HAKI ZA WATOTO


 PAPA FRANCIS

Kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi mateso imelaumu vikali kanisa Catholiki kwa kutoshughulikia ipasavyo suala la unyanyasaji wa watoto ndani ya kanisa hilo.
Katika ripoti iliyochapishwa hivi karibuni na Umoja huo mjini Geneva , Kamati hiyo imeushutumu utawala wa Vatcan kwa kuwahamisha watawa kutoka parokia moja hadi nyingine kuwaepusha kushtakiwa, na kupuuza haki za waathiriwa za kupokea fidia .
Utawala wa Vatican uliithinisha mkataba dhidi ya unyanyasaji , ukatili na matendo yaliyo kinyume na utu.Uchunguzi uliofanywa na kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi ya Vatcan ni sehemu ya uchunguzi wa mara kwa mara wa kamati hiyo dhidi ya nchi wanachama ili kuhakikisha mikataba inatekelezwa.

Kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa ina hofu kuwa wakati utawala wa Vatcan umeelezea kutokubali kamwe kuwepo kwa unyanyasaji ndani ya kanisa, maneno hayaendani na vitendo .

Kamati hiyo imekasirishwa zaidi na kwamba Utawala wa Vatcan unasisitiza kuwa unahusika zaidi na wahudumu wanaofanyika kazi ndani ya Vatcan kwenyewe , kuliko makasisi wake wanaofanyika kazi kwingineko duniani.

Mwezi Januari mwaka huu utawala wa Vatcan ulichunguzwa upya na kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto, baada ya kupokea ukosoaji kama huo kwamba ulishindwa kuwalinda watoto waliokuwa chini ya uangalizi wake.

 GERMAIN KATANGA JELA MIAKA 12

Germain Katanga

Mahakama ya kimataifa ya jinai ICC imemhukumu kiongozi wa zamani wa wanamgambo waasi katika Jamuhuri ya kidemokrasi ya Kongo, Germain Katanga, kifungo cha miaka kumi na miwili jela baada ya kumpata na hatia ya uhalifu wa kivita. 
 
Bwana Katanga alipatikana na hatia ya kuhusika katika mauaji ya mamia ya wanavijiji katikaeneo la Ituri Katanga mwezi Machi mwaka 2003.

Jimbo la Katanga ni jimbo lenye utajiri wa madini ya dhahabu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo . Lakini kiongozi huyo wa waasi mwenye umri wa miaka thelathini na sita hakupatikana na hatia ya kuwatumikisha watoto vitani na makosa mengine ya ubakaji.

Monday, 28 April 2014

 MZOZO WA KIDIPLOMASIA
 KATI YA KENYA NA SOMALIA


Mzozo wa kidiplomasia unanukia kati ya Kenya na Somalia baada ya polisi kumkamata kimakosa mmoja wa maafisa wakuu wa ubalozi wa Somalia nchini Kenya Siyad Mohamud Shire .

Tayari balozi wa Somalia nchini Kenya Mohamed Ali Nur ameitwa na serikali yake kueleza matukio yanayoambatana na kukamatwa kwa raiya wa asili ya kisomali ambao serikali inasema baadhi yao hawana vibali vya kuishi nchini.

Maafisa wa polisi nchini Kenya wamekuwa wakiendelea na msako wao dhidi ya wahamiaji haramu na wale wanaoshukiwa kushiriki matendo ya kigaidi na uhalifu.
Hata hivyo serikali ya Somalia imesikitishwa nao kwa kumkamata afisa wa ubalozi wa Somalia anayeshughulikia masuala ya kisiasa Siyad Mohamud Shire.

Kwa sababu hiyo Somalia imetuma taarifa katika vyombo vya habari ikisema kuwa waziri mkuu Abdiweli Sheikh Ahmed amefanya mazungumzo na balozi wa Somalia nchini Kenya aliyefika Mogadishu hapo Jumapili kumweleza hatma ya raiya wa Somalia wanaoishi Kenya katika msako unaoendelea.

Japokuwa serikali ya Kenya kupitia kwa wizara ya usalama wa kitaifa imekuwa ikishikilia kuwa hailengi jamii yoyote katika kuwakamata raiya wa kigeni na kuwarejesha katika nchi zao ama kambi za wakimbizi.Taarifa hiyo imeanusha hilo na kusema maafisa wa polisi wamekuwa wakiwazuilia wasomali wengi na kuwatesa.

Tukio la kumnasa, Bwana Siyad Mohamud Shire limechukuliwa na serikali ya Somali kuwa ukiukaji mkubwa wa mkataba wa kidiplomasia.Inasemekana kuwa bwana Shire alikamatwa na kuzuiliwa na polisi kwa muda licha ya kuwa na kitambulisho cha kazi.

Mkutano kati ya waziri mkuu wa wa Somali na balozi wa Kenya ulifanyika baada ya baraza la mawaziri kuandaa kikao kisichokuwa cha kawaida kujadili hali ilivyo Kenya.

Juhudi za kumpata waziri wa mambo ya nje wa Kenya balozi Amina Mohamed kueleza msimamo wa serikali hazikufaulu ila maafisa wa polisi walikataa kuzungumzia suala hilo wakisema kuwa litashughulikiwa na ngazi ya juu.

Polisi nchini Kenya walianza msako kote nchini wiki tatu zilizopita baada ya matukio mengi yanayoambatanishwa na ugaidi ama uhalifu kutokea huku zaidi ya watu kumi wakifariki baada ya milipuko kadhaa kutokea katika mtaa wa Eastleigh na maeneo jirani jijini Nairobi.

Kisichojulikana kwa sasa ni namna nchi zote mbili zitakavyoendelea kushirikiana kidiplomasia katika mazingira yaliyopo.

 

683 WAHUKUMIWA KIFO MISRI



Jaji wa mahakama nchini Misri, amewahukumu kifo watu 683 akiwemo kiongozi wa kundi la Muslim Brotherhood Mohammed Badie.
Mawakili wa watuhumiwa wanasema kuwa wateja wao walikabiliwa na makosa mengi yakiwemo, kushambulia kituo cha polisi mjini Minya mwaka 2013 ambapo polisi mmoja aliuawa.
Jaji huyo pia alibatilisha hukumu ya kifo iliyotolewa kwa watu 492 kati ya watu 529. Hukumu hiyo ilipitishwa mwezi Machi na sasa watahudumia kifungo cha maisha jela.
Kesi na kasi ya kuzisikilizwa kwa kasi hizo, imesababisha hasira na kukosolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Umoja wa Matifa UN.

Kadhalika shirika la Huma Rights Watch limelalamika kuwa kesi hizo zilisikilizwa tu kwa saa chache huku mahakama ikiwazuia mawakili kuwawakilisha washitakiwa.
Duru zinasema kuwa jamaa wa watuhumiwa waliokuwa wanasubiri nje ya mahakama walizirai baada ya kupokea taarifa za hukumu hiyo.

Mwezi jana shirika la kutetea haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, lililaani kesi hizo likisema kuwa zinakiuka sheria ya kimataifa ya haki za binadamu.
Msemaji wa shirika hilo, Navi Pillay, alisema kuwa kesi hiyo ilikumbwa na makosa mengi ya utarataibu.

Maafisa wa utawala nchini Misri wamekuwa wakiwasaka na kuwakamata wapiganaji wa kiisilamu na wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood ambao walimuingiza mamlakani aliyekuwa Rais Mohammed Morsi ambaye baadaye aliondolewa na Julai.
Mamia wameuawa huku maelfu ya raia wakikamatwa.

Monday, 7 April 2014

 DK BALALI AMVAA MAALIM SEIF

 

Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema serikali ya mkataba haiwezi kuleta maendeleo nchini, bali ni kujidanganya na kujirudisha nyuma kimaendeleo.Aliyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi na wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho katika viwanja vya Demokrasia Kibandamaiti, visiwani hapa.


Alisema serikali tatu haziwezi kutatua kero za Muungano, hivyo CCM itahakikisha inaendeleza mfumo wa Muungano wa serikali mbili.
“Tunaendelea kupigania serikali mbili. Tunafanya hivyo kwa sababu tunaipenda Zanzibar na Tanzania yetu,” alisema Dk. Bilal.


Aliwataka Wazanzibar kutokuwa na hofu kwa kuwapo kwa serikali mbili kwamba watamezwa na Muungano na kuwatoa wasiwasi kuwa Muungano hautaibeza Zanzibar.
Alisema Tanganyika na Zanzibar zimeonyesha mfano mzuri wa kumkomboa Mwafrika kwa kuunganisha nchi mbili na kuwa Tanzania, kwani nchi nyingi zilikuwa zikitafuta umoja huo lakini zilishindwa.


 “Leo nini kutafuta mbinu za kuutaka kuuvunja Muungano ambao umepanua fursa kwa Wazanzibari bila ya Muungano Wazanzibari tungebanana, Muungano umetusaidia kufifisha uhasama uliokuwapo ndani ya Zanzibar na kujenga umoja na kusahau tofauti zilizopo,” alisema Dk. Bilal. 


Alisema Watanzania wengi wanataka serikali mbili, hivyo watahakikisha wanaendeleza mfumo wa serikali mbili, kwani katika watu 100 asilimia ya watu 86 hawana tatizo na Muungano uliopo.Alitahadharisha kuwa Muungano hauwezi kudumu bila ya serikali mbili katika nchi zenye tofauti ya ukubwa wa nchi moja ndogo na nyingine kubwa, ni lazima kuwapo na uwiano utakaodumisha Muungano.


 Alisema CCM haitishiki na vitisho vya upinzani vinavyoashiria uvunjifu wa amani kwa lengo la kutaka kuuvunja Muungano.
Katibu wa CCM Mkoa wa Magharibi, Mwangi Kundya, alisema mfumo wa Muungano wa serikali mbili umetoa fursa ya kupanuka kwa soko la biashara, ajira na uwekezaji katika nyanja mbalimbali na kuimarisha huduma za kijamii ikiwamo elimu, afya na umeme.


 Alisema hotuba ya Katibu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, aliyoitoa hivi karibuni katika mkutano wa hadhara ilionyesha kukata tamaa, baada ya kuona dereva makini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuonyesha na kuweka bayana mitego yote ambayo wao walitamani Tanzania iingie. 


“Dereva huyo baada ya kuwaonyesha wajumbe wa Bunge la Katiba mitego hiyo sasa wana hakika hawawezi kufanikiwa nia yao ila wanaona bora litote tugawane mbao,” alisema Kundya.


Aliwataka wajumbe wa Bunge la Katiba kutambua dhima waliyonayo ya kuulinda, kuutetea Muungano na kutotazama takwimu zilizotolewa kwa ufinyu wake, bali wazichambue na kuzitazama kwa upana wake ili kubaini Watanzania wanachokitaka.

RWANDA YAADHIMISHA MAUAJI YA KIMBALI



Rwanda inaadhimisha miaka 20 tangu kutokea mauaji ya kimbari mwaka 1994.
Watu laki nane waliuawa wengi wakiwa wa kabila la Tutsi na Wahutu wenye msimamo wa kadri. Wote waliuawa na watutsi wenye msimamo mkali.

Hii leo Rais Paul Kagame anatarajiwa kuwasha mwenge ambao utasalia hivyo kwa siku 100 ,kipindi ambacho mauaji ya kimbare yalifanyika.Mgogoro wa kidiplomasia umesababisha Waziri wa sheria wa Ufaransa, kujiondoa katika shughuli za kumbukumbu ingawa Ufaransa inasema kuwa balozi wake ataiwakilisha nchi hiyo.

Wengi wa waathiriwa wa mauaji ya Rwanda, walishambuliwa kwa mapanga kwa siku 100. Mauaji hayo yalianza Aprili mwaka 1994, punde baada ya kufariki kwa hayati Rais Juvenal Habyarimana.

Alifariki wakati ndege yake iliposhambuliwa katika anga ya Kigali na kudunguliwa.
Baadhi ya viongozi wa kidini walihusishwa na ghasia zilizofuata kifo cha Habyarmana.
Mauaji ya kimbari yaliisha mwezi Julai 1994 wakati chama cha RPF, kilichokuwa cha waasi wa Tutsi wakati huo, kilipoingia nchini humo kutoka Uganda na kuchukua uongozi wa nchi hiyo.

Kumbukumbu zinaanza kwa kuwekwa mauwa katika eneo la kumbukumbu ya mauaji hayo na kufuatiwa na kuwashwa kwa mwenge katika uwanja wa michezo wa Amahoro mjini Kigali.Mwenge huo umekuwa ukitembezwa katika nchi hiyo kwa miezi mitatu iliyopita

Viongozi wa kimataifa akiwemo waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair,aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Thabo Mbeki na katibu mkuu wa UN Ban Ki-moon wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo.Mnamo Jumapili mamia ya watu walihudhuria maombi kuwakumbuka maelfu waliouawa .

WAUKRAINE WANAOUNGA MKONO URUSI WAVAMIA MIJI


Rais wa Mpito wa Ukraine, Oleksandr Turchynov, ameitisha mkutano wa dharura wa maafisa wake wa usalama baada ya waandamanaji wanaounga mkono Urusi kuvamia na kuingia katika Ofisi za Serikali katika miji mitatu Mashariki mwa Ukraine.
Miji ya Donetsk,Kharkiv na luhansk, ndiyo imeshuhudia maandamano makubwa zaidi .
Waandamanaji walikabiliana na maafisa wa polisi na kuziweka bendera za Urusi katika makao makuu ya miji hiyo .

Wanadai wanataka kufanyike kura ya maoni ili na wao wafuate mkondo wa rasi jirani ya Crimea kujitenga na Ukraine .Serikali ya Kiev imeishtumu Urusi kwa kuchochea ghasia hizo iliipate fursa ya kuivamia Ukraine kijeshi kwa niya ya kuigawanya.

Kaimu waziri wa usalama wa taifa wa Ukraine Arsen Avakov amesema polisi tayari wamewaondoa waandamanaji ambao walikuwa wamepora silaha kutoka kwenye handaki kuu ya jimbo la Kharkiv.

Matukio hayo yamevutia hisia kali kutoka kwa mataifa jirani ,Rais wa jamhuri ya Czech Milos Zeman amesema kuwa vikosi vya NATO vinafaa kujiandaa kuivamia Urusi kwa kuingilia kijeshi mashariki mwa Ukraine.

Katibu mkuu wa NATO, Anders Fogh Rasmussen, amenukuliwa akiiambia gazeti la The Daily Telegraph kuwa Urusi inajaribu kuibua makanda yenye ushawishi barani Uropa.

WAASI NCHINI LIBYA WAKUBALI MAFUTA YAUZWE


Makubaliano yameafikiwa kuondoa kizuizi cha kusafirisha mafuta mashariki mwa Libya. Mauzo ya mafuta katika nchi za ng'ambo nchini humo yaliathirika pakubwa katika kipindi cha miezi minane iliyopita baada ya kufungwa kwa bandari zilizo katika eneo la mashariki linalotawaliwa na makundi ya wanamgambo.

Katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyiwa katika jiji la Beghazi, Waziri wa Maswala ya Haki wa Libya, Salah Al-Maghani, alithibitisha kuondolewa kwa muda kwa vizuizi vya kuuza mafuta.
Vituo vya mafuta vya Hureiga na Zuetina vilivyo na uwezo wa kuzalisha mafuta mapipa 200,000 kwa siku hivi sasa vimesimamiwa na Serikali.Vituo viwili vilivyo vikubwa zaidi nchini humo vya Mashariki mwa nchi vya Ras Lanuf na Sidra vitafunguliwa kwa muda wa majuma machache yajayo, kulingana na Waziri.

Mapatano yaliafikiwa kati ya makundi ya wapiganaji yaliyosababisha kufungwa kwa vituo hivyo na kundi ambalo Serikali ililitaja kama "wapatanishi". Msemaji wa Waziri Mkuu ameambia BBC kuwa Serikali imekubali kuwalipa mishahara walinzi wa vituo hivyo vya mafuta.Juhudi za mwezi uliopita za kufikia mapatano ya kuanza kuuza mafuta tena katika vituo hivyo hazikufaulu.

Wale wanaozuia mafuta kuuzwa katika vituo hivyo wamekuwa wakilalamika kuwa sekta ya mafuta nchini Libya inakabiliwa na ufisadi mkubwa, lawama ambayo imekanushwa na maafisa wa Serikali.

Wapiganaji hao pia wamekuwa wakisema kuwa wakaazi wa Mashariki wanahitaji mapato makubwa zaidi kutoka kwa mauzo ya mafuta. Waziri wa Haki sasa anasema kuwa Serikali itachunguza lawama za ufisadi.

Libya imepata hasara ya zaidi ya Dola Bilioni tisa tangu kufungwa kwa vituo hivyo vya mafuta. Eneo la Mashariki ndilo linalozalisha kiwango kikubwa cha mafuta.

Friday, 28 March 2014

NI SERIKALI MBILI AU TATU WAAMUE WABUNGE

 KIKWETE ASEMA TUWAACHE WABUNGE WAAMUE SERIKALI MBILI AU TATU

 

Rais Jakaya Kikwete amesema amemaliza  kazi ya kulihutubia Bunge Maalum la Katiba na sasa anawaachia wabunge wa bunge hilo kujadili na kuamua muundo wa Muungano unaofaa kama serikali mbili au tatu kwenye mapendekezo ya  Rasimu ya Katiba Mpya.


Rais Kikwete alielezea msimamo huo juzi wakati akizungumza na wazee  katika Ikulu ndogo ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.

Rais Kikwete ambaye alikuwa katika ziara yake ya siku moja wilayani hapa, alitoa msimamo wake baada ya wazee hao kumweleza kwenye risala yao kuwa wao wanataka serikali mbili. Risala hiyo ilisomwa na   Mwenyekiti wa Wazee wa Wilaya ya Muheza, Hamisi Mzee.

Rais Kikwete alisema kwa sasa amewaachia wabunge kuamua muundo wa Muungano unaotakiwa na baadaye wananchi wataamua kama wanataka serikali tatu ama mbili wakati wa kupitisha Katiba.

Alisema kama watapendekeza serikali tatu ruksa kwani ndiyo mapendekezo yao, hivyo hayawezi kupingika kwa namna yoyote.

Hata hivyo, Rais Kikwetee alisisitiza kuwa lakini waelewe kuwa serikali tatu zina changamoto zake

 POLISI WAUA DEREVA WA BAJAJI KWA KIPIGO

 

Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni limeingia katika kashfa baada ya askari wake wa Kituo cha Stendi Kikuu ya Mabasi Ubungo (UBT), kutuhumiwa kumpiga, kumjeruhi na kusababisha kifo cha dereva wa bajaji, Salehe Said (19), maarufu kama ‘Kibange Moto’, mkazi wa Kigogo, jijini Dar es Salaam.
Dereva huyo alikutwa na mkasa huo, Machi 24, mwaka huu, saa 7:00 usiku, huku kukiwa na utata wa eneo alilokutwa na mauti.

Utata huo unafuatia polisi kudai kuwa dereva huyo alifariki wakati akiendelea na matibabu, huku kikundi cha madereva wa bajaji cha Jitume cha Ubungo kikidai kuwa alifia mikononi mwa polisi.

 Baadhi ya madereva wa bajaj walidai chanzo cha tukio hilo ni ugomvi kati ya marehemu na dereva teksi bubu uliotokana na kugombea abiria aliyefika katika eneo hilo kutafuta usafiri nje ya UBT.

Walidai kutokana na vuta nikuvute hiyo, wote wawili walikamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi.

Kwa mujibu wa madereva hao, Saleh aligoma kuingia mahabusu ya kituo hicho akitaka kwanza aambiwe kosa lake.

Walidai jambo hilo lilisababisha askari huyo (jina linahifadhiwa) kuanza kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kuwa baada ya kipigo hicho, baadhi ya madereva wenzake walianza kumtetea, lakini nao walikamatwa na kuwekwa ndani.

Walidai baada ya muda mfupi, mwenzao aliyepigwa alianza kuvimba na polisi aliyempiga aliamua kumpeleka katika Hospitali ya Sinza Palestina, lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya.

“Wakati askari huyo amempiga dereva mwenzetu, walikamatwa wengine watano wakawekwa ndani, lakini hali ya mwenzetu ilipokuwa mbaya, askari walimchukua na kumpeleka katika Hospitali ya Palestina Sinza, lakini walipomrudisha kituoni, alizidiwa. Wakamrudisha tena hospitali usiku huo huo,” alisema mmoja wa madereva hao.

Aliongeza: “Mara ya kwanza walivyompeleka hospitali, walitumia bajaj ya mwenzetu, ambaye naye alikuwa amewekwa ndani, lakini mara ya pili hali ilipozidi kuwa mbaya, walimrudisha hospitali na hawakumrudisha tena kituoni.”

 Kijana huyo alisema Jumanne asubuhi baada ya kwenda kituo cha polisi cha UBT walikokuwa wameshikiliwa wenzao, waliambiwa kuwa walikuwa wamehamishiwa kituo cha Magomeni Usalama.

Alisema baada ya kwenda kituo cha Usalama, waliwakuta wenzao wanne, ambao waliwaeleza kwamba, mwenzao aliyekuwa amepigwa alipelekwa hospitali usiku na hakurudishwa tena kituoni.

 Alisema walipowauliza polisi mwenzao aliko, hawakutoa jibu lolote na ndipo waliamua kufuatilia katika hospitali waliyokuwa wamempeleka, lakini hawakumuona na hivyo kuanza kumtafuta katika hospitali nyingine.

“Tulipokosa jibu la wapi alipo mwenzetu kutoka kwa askari, tuliamua kutembelea kila hospitali. Tulipofika Mwananyamala kwenye wodi, napo tulimkosa. Tukaamua kwenda mortuary (chumba cha kuhifadhi maiti). Tukakagua daftari na ndipo tukaona jina lake,”  alisema.

Aliongeza: “Kwa kweli ilituuma sana. Tena kibaya zaidi, maelezo yalikuwa yameandikwa kuwa kifo chake kimesababishwa na kupigwa.
Tunaomba sheria ichukue mkondo wake huyo askari achukuliwe hatua kali. Na pia tunataka wenzetu waliokamatwa bila hatia, waachiwe kwa sababu polisi wamewabambikia kesi ya wizi wakati siyo kweli.Pia faili lake limeandikwa kwamba alipigwa na wananchi wenye hasira kali, tumechoka kuonewa.”
Juzi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema hana taarifa zozote juu ya tukio hilo.Hata hivyo, jana alipoulizwa tena alisema: “Kifo cha dereva huyo hakikusababishwa na askari.”

Wambura alisema dereva huyo alikamatwa na kufikishwa kituoni kwa tuhuma za kumvamia afisa wa Benki ya ABC na kumpora na kuwa baada ya kukamatwa, alijaribu kutoroka, lakini alikamatwa tena na polisi kwa kushirikiana na watu wengine na kurudishwa kituoni.

“Kwanza naomba unielewe kwamba kifo cha dereva huyo, ambaye pia inasemekana ni ‘deiwaka’ wa bodaboda hakikusababishwa na polisi.
Bali alitaka kuwatoroka polisi baada ya kukamatwa kutokana na kosa la kumvamia afisa wa ABC katika lango la kutokea stendi ya mkoa (UBT) na kikundi cha madereva wanaopaki katika eneo hilo. Na kati ya waliohusika na tukio hilo, ni pamoja na huyo marehemu,” alisema Wambura.
Alisema afisa huyo aliegesha gari lake akisubiri mgeni wake, lakini kikundi hicho kilimzongazonga na kuanza kumshambulia kisha kumpora Sh. 40,000, simu mbili na kadi za benki na kumchania nguo zake.

Wambura alisema afisa huyo aliripoti kituo cha polisi na baadaye askari walikwenda kuwakamata madereva hao.

Alisema majira ya saa 4:30 usiku, marehemu alizidiwa na kupelekwa katika Hospitali ya Palestina Sinza.

Kwa mujibu wa Wambura, marehemu alirudishwa kituoni, lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya, hivyo kulazimika kurudishwa tena hospitalini hapo na baadaye Hospitali ya Mwananyamala na kwamba, ilipofika saa 7:00 usiku alifariki.

Wambura alisema kutokana na madai mbalimbali, wanafanya uchunguzi kujua chanzo hasa cha kifo hicho.

TALIBAN YAISHAMBULIA KABUL

 

Wanamgambo nchini Afghanitan wameshambulia jumba moja la kukodi lililo karibu na majengo ya bunge kwenye mji mkuu Kabul .
Mwandishi wa BBC mjini Kabul anasema kuwa baada ya mlipuko mkubwa kusika mapigano yalifuata.

Jumba hilo lilitumiwa na wageni kutoka mataifa ya kigeni lakini mkuu wa polisi alisema kuwa hakukuwa na wageni wakati wa tukio hilo.

Kundi la Taliban limesema ndilo lilioendesha shambulizi hilo llikiwa moja ya mashambulizi kadha ambayo yameshuhudiwa wiki hii.

Kundi la Taliban limeapa kuwa litavuruga uchaguzi wa urais ambao utaandaliwa mwezi ujao nchini Afghanistan.

Thursday, 27 March 2014

RAISI OBAMA KUKUTANA NA PAPA ROMA

 

Rais Barrack Obama wa Marekani anatarajiwa kukutana na kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, katika makao yake makuu huko Vatican.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Obama kukutana na papa Francis.

Wawili hao wanatarajiwa kujadili namna ya kupunguza tofauti iliyopo kati yao katika maswala mengi mbali na kujaribu kuinua maisha ya watu maskini duniani baada ya takwimu kuonyesha kuwa tofauti ya mapato kati ya matajiri na Masiki inaendelea kupanuka .

Aidha viongozi hao wawili wanatazamiwa kujadili hali ilivyo Nchini Ukraine, na swala la upatikanaji wa amani mashariki ya kati.

Mwafaka baina ya mitazamo tata kuhusiana na maswala ya uavyaji mimba, matumizi ya dawa za kupanga uzazi na ndoa ya jinsia moja pia inatarajiwa kuwa kati ya mada itakayojadiliwa .

UN YAILAANI MISRI KUHUSU HUKUMU YA KIFO

 

Umoja wa Mataifa umelaani kitendo cha Misri kuwahukumu kifo zaidi ya watu miatano ikisema kuwa ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa za haki za binadamu.

Umoja huo umesema kuwa idadi ya watu waliohukumiwa Jumatatu, ndio idadi kubwa ya watu kuwahi kuhukumiwa kifo kwa wakati mmoja katika miaka ya hivi karibuni.

Mawakili wa utetezi wamesusia kesi ya pili ya watu wengine karibu miasaba wafuasi wa Morsi wanaokabiliwa na tuhuma sawa na zile zilizowakabili watuhumiwa wa kwanza.
Wamlalamikia kile wanachosema ni mahakama kukosa kufuata utaratibu unaofaa.

Kesi ya wafuasi wengine 682 waliosalia ilianza kusikilizwa mapema leo lakini ikaahirishwa baada ya muda mfupi huku jaji akisema kuwa hukumu itatolewa mwezi ujao.

MKUU WA JESHI KUGOMBEA URAISI MISRI



Mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi Misri, Abdul Fattah al-Sisi, ametangaza kujiuzulu jeshini ili kugombea katika uchaguzi wa urais mwezi ujao.
Wagombea wote wanapaswa kuwa raia.
Akizungumza Kwenye hotuba ya Televisheni huku akiwa amevalia sare ya kijeshi Abdel Fattah El Sissi amesema yeye sio mwanajeshi tena baada ya miaka 44 na kwamba amechukua hatua hiyo ili aweze kutimiza jukumu lingine muhimu.

Ni Bayana kwana Sisi hatakua na kibarua kigumu kujipatia ushindi katika uchaguzi wa Urais. Anaungwa mkono na idadi kubwa ya raia wa Misri na hadi sasa hana wapinzani wowote.
Baadhi ya waliotaka kugombea urais wamejiondoa wakidai kwamba hawataweza kuendesha kampeni zao kwa njia huru.

Wafuasi wake Sisi wanamuona kama kiongozi imara ambaye anaweza kurejesha amani na udhabiti nchini Misri baada ya miaka mingi ya machafuko.
Wakosoaji wake wanasema ana msimamo mkali na amechangia pakubwa katika kusambaratisha na kuhujumu upinzani nchini Misri.

Mkuu huyo wa jeshi atakabiliwa na majukumu mazito ya kufufua uchumi uliofifia , kupambana na uasi na kuileta pamoja nchi iliyogawanyika. Ameahidi kutekeleza mabadiliko makubwa lakini akaonya kuwa hawezi kufanya miujiza.

Tuesday, 25 March 2014

 MGOMO WA DALADALA MOSHI


 

Vurugu  kubwa zimezuka katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi na kusababisha gari lililowabeba askari kanzu wa Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kupopolewa kwa mawe na kisha kuvunjwa vioo na watu wanaodaiwa kuwa wafanyakazi wa mabasi yanayotoa huduma  hiyo katika miji ya Arusha na Moshi.


Vurugu hizo zilitokana na wamiliki wa mabasi pamoja na madereva kugoma kutoa huduma kuanzia asubuhi saa 11 hadi saa 10:30 jioni wakilalamika kuwa wanalazimishwa na askari wa kikosi cha usalama barabarani kutoa rushwa ili kuficha makosa baada ya kuwadai stakabadhi ya uthibitisho wa malipo wanayotoa kwa askari hao.


Gari la Polisi lilipopolewa kwa mawe na kuvunjwa vioo likiwa na askari kadhaa ni lenye namba za usajili T 743 ADC Toyota Land Cruiser, lilikumbana na dhoruba hiyo baada ya askari kujaribu kumkamata mmoja wa madereva wa mabasi hayo ambaye hakufahamika jina mara moja anayefanya safari kati ya Moshi Mjini na Holili mpakani mwa Tanzania na Kenya.


Kufuatia mgomo huo, abiria wanaosafiri katika miji ya Arusha, Moshi na wilaya sita za mkoa wa Kilimanjaro walikwama kwa kutwa nzima jana.


 Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji wa Mabasi Kanda ya Kaskazini (Akiboa), Hussein Mrindoko, wamesema kua wameamua kugoma kutokana na baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani kugeuza stakabadhi za malipo yanayotokana na faini kuwa mtaji wa kibiashara kwa kuwa wanatoza gari moja faini ya Sh. 30,000 hadi mara tatu kwa siku.


 “Tunakuomba Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa (Leonidas Gama) uchukue hatua za kimaadili dhidi ya maofisa watatu wa Jeshi la Polisi ambao wamekuwa wakifanya maamuzi ya kibabe na kusababisha uzaliwe mgogoro huu. Huyo ofisa anayekojoa nyuma ya magari halafu amelewa ni fedheha kwa jeshi na serikali kwa ujumla,” alisema Mrindoko katika kikao alichoitisha mkuu huyo wa mkoa.


Wakiwa katika mkutano huo wa usuluhishi, baadhi ya madereva hao na wamiliki wa mabasi walimweleza Gama kwamba Mkuu wa kikosi hicho, Mkuu wa kituo kidogo cha Polisi cha Stendi Kuu ya Mkoa na Mkaguzi wa Polisi kituo cha Himo wamekuwa na desturi ya kufanya kazi kwa ubabe ikiwamo kuwapiga makonde na kuwabambikizia makosa baada ya kuhoji uhalali wake, hivyo kusababisha uhasama mkubwa.


 Akijitetea, Mkuu  wa Kikosi cha Usalama Barabarani (RTO), Joseph Mwakabonga, alikiri kumpiga makonde mmoja wa wamiliki wa mabasi wa wilaya ya Hai,  Abdulrazack Mtoro, akidai sheria inamruhusu kufanya hivyo pale kunapokuwa na vurugu.


Kwa upande wake, Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi Stendi Kuu (OSC), Hendry Nguvumali, alisema madereva na wamiliki wa mabasi hayo wanashuhudia uongo kwa kumdanganya mkuu wa mkoa kwamba yeye ni mlevi wa kupindukia na amekuwa akikojoa nyuma ya mabasi ya abiria, jambo ambalo haliwezi kumzuia kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria.


Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, akizungumzia malalamiko yanayotokana na kupotoka kwa maadili ya askari, alisema ofisi yake itachukua hatua za kimaadili haraka iwezekanavyo, ingawa wananachi pamoja na madereva wa mabasi hayo wanatakiwa pia kutii sheria za usalama barabarani bila kushuruti.


 “Nitachukua hatua mara moja kuhusu maadili, hili la ulevi wa kupindukia kwa kweli limelidhalilisha Jeshi la Polisi, lakini pia suala la kupiga watu makonde siyo utaratibu kwa sababu ofisa anatakiwa kufuata sheria na kwa kuwa amekiri mwenyewe (RTO) nitalitazama kwa kufanya uchunguzi,” alisema Boaz.


Gama alisema iwapo mgomo huo wa mabasi utaachwa uendelee kwa siku ya pili, unaweza ukasababisha kuporomoka kwa uchumi wa mkoa huo.  Gama aliamuru Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kupeleka ofisini kwake ratiba inayoonyesha namna anavyokutana na wadau wa usafirishaji pamoja na kushughulikia kero zinazotokana na askari wa usalama barabarani.


 “Nyie Polisi, Sumatra na wasafirishaji mnafanya kazi zenu kwa kuviziana na kutengenezeana uhasama ili kuonyeshana ubabe. Muda mfupi baada ya kukaa na kamati yangu ya ulinzi na usalama, nitatoa taarifa kwa umma kuhusiana na hatua za kinidhamu nilizochukuliwa kama serikali kwa niaba ya Waziri Mkuu,” alisema Gama na kuongeza:


 “Sumatra nataka mnieleze kwa nini agizo langu hamjatekeleza hadi sasa na mmezalisha mgogoro huu?”
Mgomo huo ulisababisha wananchi kutumia usafiri wa bodaboda, bajaj na magari madogo ya kukodi. Hawa Hussein, mkazi wa Rombo alisema mgomo huo uliathiri shughuli zake nyingi za kiuchumi.


Francis Meena, mkazi wa Sanya Juu alisema mgomo huo ulisababisha adha kubwa ikiwamo kutembea kwa miguu umbali mrefu huku wengine wakilazimika kuingia gharama za kukodi bodaboda kwa gharama ya Sh. 5,000.
Mkaguzi mmoja aliliambia gazeti hili kuwa magari hayo yanastahili kukamatwa na trafiki kwa kuwa mengi ni mabovu na yanakiuka sheria za barabarani.


Alizitaja kuwa ni kupakia abiria katika maeneo yasiyo rasmi, hayafanyiwi usafi na kutokidhi viwango vya magari ya abiria.
Alisema wamiliki wake wanalalamikia, magari yao kukamatwa, lakini wana makosa mengi ya kiusalama.


 “Ninakuambia katika magari 300 ni magari 20 yatakidhi vigezo vya kubeba abiria kama yakikaguliwa sawasawa,” alisema mkazi mmoja wa mjini Moshi aliyejitambulisha kama msafiri wa kila siku ndani ya mkoa wa Kilimanjaro.

URUSI YATENGWA NA G7

 


Viongozi wa kundi la mataifa saba tajiri zaidi duniani, G-7, wanafanya mazungumzo kwa siku ya pili mfululizo hivi leo mjini Hague, Uholanzi ajenda kuu ikiwa ni hatua ya Urusi kunyakua jimbo la Crimea kutoka Urusi.

Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1998, Moscow imenyimwa kiti katika kongamano hilo. Mkutano wa dharura wa G-7 uikubaliana kufutilia mbali kundi la G-8, kundi la mataifa manane tajiri zaidi duniani, ambalo linaishirikisha Urusi.

Viongozi wa mataifa ya kundi hilo wameonya kuwa vikwazo zaidi vitatolewa iwapo Urusi itaingia maeneo ya mashariki au Kusini mwa Ukraine ikiwepo kulenga sekta ya kawi nchini Urusi. Lakini Marekani kadhalika imesisitiza kuwa fursa ya kusuluhisha mzozo huo wa njia ya kidiplomasia ingalipo.